Jumatano, 30 Rabi' al-thani 1447 | 2025/10/22
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Mfuko wa Fedha wa Kimataifa wafikia Kukaba Uchumi wa Yemen ili Kukamata Rasilimali Zetu za Kiuchumi

Mnamo tarehe 15/10/2025, Gavana wa Benki Kuu ya Aden, Ahmed Al-Maabqi, alikutana jijini Washington D.C., na mkuu wa ujumbe wa Mfuko wa Fedha wa Kimataifa (IMF) nchini Yemen, Esther Pérez Ruiz, na mwakilishi wa IMF, Mohamed Maait, akiandamana na Naibu Waziri wa Fedha Hani Wahab na Msaidizi wa Katibu Mkuu wa Waziri Msaidizi wa Fedha Abdul Qader Amin. Hii ilifuatiwa na mkutano kati ya Waziri wa Mipango na Ushirikiano wa Kimataifa na Gavana wa Yemen kwa Benki ya Dunia, Waed Badhib, na Riccardo Puliti, Makamu wa Rais wa Shirika la Fedha la Kimataifa wa Kanda ya Mashariki ya Kati, pamoja na ushiriki wa Naibu Waziri wa Mipango Nizar Basuhaib, Naibu Waziri wa Fedha Hani Wahab, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha Abdul Qader Amin, kwa uwepo wa Stefan G. G. Reimbert, Mkurugenzi wa Kanda wa Benki ya Dunia katika Mashariki ya Kati, na Dina Abu Ghaida, Meneja wa Benki ya Dunia nchini Yemen.

Soma zaidi...

Msimamo kwa Sherehe za Maadhimisho ya Mapinduzi Mawili ya Septemba Moja yaliingiza Usekula nchini Yemen na Mengine Yalitoa Wito wa Kuuimarisha!

Katika mwezi wa Septemba wa kila mwaka Yemen ina matukio mawili; la kwanza mnamo tarehe 26 Septemba 1962 ambayo ni kumbukumbu ya kupinduliwa kwa mfumo wa kifalme nchini Yemen Kaskazini, na la pili mnamo tarehe 21 Septemba 2014 ambayo ni kumbukumbu ya kuingia kwa Mahouthi jijini Sana’a ambayo ilisababisha udhibiti wao wa mikoa ya kaskazini.

Soma zaidi...

Chama cha Jumuiya ya Mageuzi ya Yemen (Islah), Sura ya Kiislamu ya Serikali Inayodai kuwa ni ya Kiislamu, Lakini iko Mbali Nao!

Mohammad Abdullah Al-Yadoumi, Mwenyekiti wa Baraza Kuu la chama cha Jumuiya ya Mageuzi ya Yemen (Islah), alitoa hotuba Ijumaa jioni, 12/9/2025, kuadhimisha miaka 35 tangu kuanzishwa kwa chama hicho, ambayo ilikuwa Septemba 13. Hotuba hiyo, iliyopeperushwa na Suhail TV na kudumu kwa zaidi ya dakika  arubaini, ilijumuisha msimamo wa chama hicho juu ya masuala ya ndani na ya kimataifa.

Soma zaidi...

Chuki na Uhalifu wa umbile la Kiyahudi mjini Gaza na Yemen Haitakomeshwa isipokuwa kwa Khilafah Rashida ya Pili kwa Njia ya Utume, Mlinzi wa Matukufu ya Waislamu

Kulengwa kwa Yemen na umbile la Kiyahudi kusingetokea isipokuwa kwa kukosekana utawala wa Uislamu, na kutabanniwa kwa sheria ya kimataifa inayowakilishwa na Umoja wa Mataifa na wale walio nyuma yake kama kibla chao, na malipo kama hayo ya kuacha kutawala na Uislamu ni matokeo ya kutarajiwa tu – hadi wanasiasa wa Yemen waregee kwenye fahamu zao na kuuweka Uislamu katika utabikishaji ndani ya Khalifah ya pili kwa njia ya Utume.

Soma zaidi...

Wakati Mahouthi Wakishangilia Uhamasishaji wa Makabila ya Bakil na Hashid na Kupigwa kwa Ngoma za Vita Baina Yao!

Mnamo Jumamosi, 26/07/2025, Sheikh Hamid Mansour Radman aliuawa katika eneo la Al-Hayit, Wilaya ya Ayal Surayh, katika Mkoa wa Amran, na mkwe wake, Hamir Saleh Rattas Falyatah (Abu Udhr) mkuu wa idara ya polisi ya Al-Hayit. Mauaji ya Sheikh Radman yalikuja baada ya kuondoka nyumbani kwake, kufuatia mzozo wa kifamilia. Muuaji anashikilia wadhifa wa mkuu wa idara ya polisi, ambaye wajibu wake ni kulinda maisha, mali, na heshima, na kuhakikisha faraja na usalama wa jamii, kuondoa shida zake, kudumisha amani kote, na kuwazuia wakjukaji na wavamizi dhidi ya maisha ya watu – sio kumuua bamkwe wake kwa kukusudia kwa kumpiga risasi kwenye barabara ya umma!

Soma zaidi...

Mafanikio ya Kiuchumi ya Mahouthi Baada ya Miaka 11: Kutengeneza Sarafu Mbili za Riyal 50 na 100!!

Mnamo Jumatatu, tarehe 14/07/2025, Waziri wa Habari wa Wizara ya Ujenzi na Mabadiliko, Hashem Sharaf al-Din, alitoa taarifa kwa Shirika la Saba, ambapo alisema: “Kila sarafu ya kitaifa inayotolewa kwa wananchi ni daraja la kuelekea katika maamuzi huru, na kila ushindi wa kiuchumi unaopatikana ni ngome isiyotikisika mbele ya dhoruba na kila mafanikio ya kifedha ni ngao ya kinga katika vita vya hadhi, na upanga unaozikata njama za maadui wa Yemen, kwa fadhila ya Mwenyezi Mungu kwanza, kisha kwa azma ya watu wasiojua lisilowezekana.”

Soma zaidi...

Haya ndiyo Matendo ya Umoja wa Mataifa... Mutaendelea Kuwahadaa Wananchi Mpaka Lini? Ni Kipi Kipya? Yako wapi Mabadiliko, Ee Wizara ya Ujenzi na Mabadiliko?

Mnamo Jumapili, tarehe 29/6/2025, jijini Sana'a, Waziri wa Masuala ya Kijamii na Leba, Samir Baja'ala, alifanya mkutano na kamati za maandalizi ya Kongamano la Vyama vya Ushirika la 2025, litakaofanyika mapema Julai 2025. Mkutano huo ulihudhuriwa na Ali Al-Razami, Katibu Mdogo wa Wizara ya Sekta ya Maendeleo na Nasser Al-Kahili, Mkurugenzi wa Afisi ya Masuala ya Kijamii na Afisi ya Leba katika Sekretarieti Kuu.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Yemen Inawapongeza Watu wa Imani na Hekima na Umma wa Kiislamu kwa Sikukuu ya Idd al-Adha iliyobarikiwa

Hizb ut Tahrir / Wilayah Yemen inatoa pongezi zake za dhati na baraka zenye thamani kubwa zaidi kwa watu wa imani na hekima, na kwa Amiri wa Hizb, mwanachuoni mkubwa Ata Bin Khalil Abu Al-Rashtah, na kwa wanachama wote wa Hizb, na kwa Ummah mzima wa Kiislamu kwa sikukuu ya Idd al-Adha iliyobarikiwa mwaka huu wa 1446 H. Mwenyezi Mungu airudishe kwao, juu yetu, na juu ya ulimwengu wote kwa kheri, baraka, na furaha.

Soma zaidi...

Sheria ya Kimataifa ni Sheria ya Pori - Hairuhusiwi Kuiendea

Chini ya ufadhili wa Daniel Capoli, Mratibu wa Masuala ya Kibinadamu katika misheni ya Kamati ya Kimataifa ya Msalaba Mwekundu (ICRC) nchini Yemen, ICRC huko Sana'a ilipanga, mnamo Jumanne na Jumatano, 20-21/05/2025, kwa ushirikiano na Wizara ya Habari na Wizara ya Mambo ya Nje, kozi ya mafunzo katika Wizara ya Mambo ya Nje kwa wafanyikazi wa vyombo vya habari na taasisi ya waandishi wa habari. Kozi hiyo ilishughulikia sheria za kimataifa, misingi na malengo yake, na istilahi zinazohusiana na sheria za kimataifa za kibinadamu, haswa katika suala la haki za binadamu katika ulinzi na maisha yenye staha, kuzuia ghasia, na kukidhi mahitaji ya vikundi vilivyo hatarini zaidi vinavyofinikwa na ulinzi wake, na vile vile kulinda raia dhidi ya athari za uhasama na kuharamisha mateso yasiyo na haja au madhara kupita kiasi.

Soma zaidi...

Wananchi Wanataka Kupinduliwa kwa Serikali na Kusimamishwa kwa Utawala wa Kiislamu

Aden, mji mkuu wa muda wa serikali ya Yemen, umeshuhudia maandamano matatu ya wanawake na wanaume katika wiki mbili zilizopita. Kutokana na mateso yanayoendelea kwa wananchi, maandamano ya hasira yamefanyika mjini Aden, wakidai huduma za msingi na kukemea hali ngumu ya maisha na huduma duni. Maandamano haya yalijumuisha kauli mbiu dhidi ya muungano wa Waarabu, serikali ya Yemeni, na Baraza la Mpito, ambalo linadhibiti mji mkuu wa muda, Aden. Maandamano haya pia yalishuhudia milio ya risasi na kukamatwa kwa baadhi ya waandamanaji. Maandamano haya yalifanywa na wanawake na wanaume kwa siku tofauti. Kilichotia fora ni kuregea kauli mbiu isemayo “Wananchi wanataka kupinduliwa kwa serikali,” ambayo inatukumbusha Mapinduzi ya Kiarabu dhidi ya ukandamizaji na udhalimu.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu