Ijumaa, 25 Rabi' al-thani 1447 | 2025/10/17
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Mauaji na Njaa ya Watoto wa Gaza Havitakwisha Kupitia Mipango ya Wale Waliohusika na Mauaji ya Halaiki Bali Kupitia Uhamasishaji wa Majeshi ya Waislamu Pekee

Katika kipindi cha miaka 2 iliyopita, watu wa Gaza wamekuwa wakikabiliwa na mashambulizi ya mabomu, mzingiro wa kikatili na jinai za kutisha zaidi za umbile la mauaji la Kiyahudi, ambapo wanawake na watoto wamekuwa wahanga wakuu. 65,000 wameuwawa, wakiwemo zaidi ya watoto 20,000 – sawa na watoto 30 wanaouawa kila siku. Watoto wamepigwa risasi kimakusudi na wavamizi wa Kiyahudi au mashambulizi ya droni barabarani, au hata wanapotafuta chakula kwenye vituo vya misaada ambavyo vimekuwa ‘mitego ya kifo’ kwa wanaokabiliwa na njaa. Kulingana na ‘Save the Children’, watoto waliuawa au kujeruhiwa katika zaidi ya nusu ya mashambulizi mabaya katika maeneo ya usambazaji wa chakula mjini Gaza ndani ya wiki nne baada ya Wakfu wa Kibinadamu wa Gaza kuanza shughuli zake.

Soma zaidi...

Enyi Waislamu: Chukueni Hatua na Msiache Masuala Yenu Yawe Mikononi mwa Maadui Zenu

Mazungumzo ya awamu ya kwanza ya mpango wa Rais wa Marekani Donald Trump kusimamisha vita dhidi ya Gaza yalianza mjini Sharm El-Sheikh nchini Misri, kwa kuhudhuriwa na wajumbe wa Marekani Steve Witkoff na Jared Kushner, Waziri Mkuu wa Qatar, na wakuu wa kijasusi wa Uturuki na Misri.

Soma zaidi...

Machozi ya Furaha kwa Maadui wa Mwenyezi Mungu, Kushindwa na Kukata Tamaa kwa Waislamu nchini Cyprus

Aprili iliyopita, Baraza la Mawaziri la Cyprus Kaskazini lilitoa “amri ya kiserikali” ambayo inaruhusu wanafunzi kuvaa hijabu za Kiislamu katika shule za sekondari. Hata hivyo, Muungano wa Walimu wa Sekondari wa Cyprus na Uturuki (KTOEOS), ulianza migomo, ukakataa kufundisha watoto waliofika shuleni wakiwa wamevalia mavazi ya kidini, na hatimaye wakaiomba Mahakama Upeo. Wiki iliyopita (mwisho wa Septemba), Mahakama ya Upeo ya Cyprus Kaskazini ilibatilisha “amri ya kiserikali”, ikiamua kuwa ilikuwa kinyume na katiba. Viongozi wa Muungano huo wa Walimu, ambao waliomba kubatilishwa kwa amri hiyo, walisherehekea kuregea kwa marufuku ya hijabu kama “ushindi kwa usekula” kwa kububujika “machozi ya furaha”. Wakati huo huo serikali imetangaza kuanza mara moja “kufanyia kazi sheria mpya”.

Soma zaidi...

Uacheni Umma Ufanye Uamuzi Wake, Enyi Watawala Waoga!

Hatukushangazwa, wala Umma wa Kiislamu haukushangazwa na ukaribishaji wa watawala wasaliti wa Waislamu wa mpango wa rais wa Marekani Donald Trump wa kuipoteza Gaza, kwani wao wametuzoezesha sisi kuwa waoga, badala ya kula njama na wakoloni makafiri dhidi ya masuala yetu. Trump alikuwa amekutana na baadhi yao jijini New York kando ya mikutano ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, mnamo Jumanne tarehe 23/9/2025, na wakamsifu na kutangaza kumtegemea yeye kumaliza vita dhidi ya Gaza. Mara tu Trump alipotangaza mpango wake wa ukoloni, waliharakisha kuukaribisha. Wasingewezaje kuukaribisha, wakati hakuna hata mmoja wao aliyesubutu kufanya vyenginevyo, kwa kuwa wamepoteza ari na ushujaa wa wanaume.

Soma zaidi...

Kutambuliwa kwa Dola ya Palestina Kutambuliwa kwa Mayahudi Kunyakua 78% ya Palestina!

Uingereza, Canada, Australia na Ureno zililitambua ile inayoitwa “Dola ya Palestina,” na kufuatiwa na nchi kadhaa katika mkutano wa ngazi ya juu wa kimataifa wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa uliofanyika kuanzia Septemba 22-30, 2025, na ulioongozwa na Ufaransa na Saudi Arabia. Utambuzi huu ulikaribishwa na watawala Ruwaibidha (wajinga wasio na maana) wa Waislamu, pamoja na Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu na Jumuiya ya Waarabu. Jambo la kushangaza ni kwamba, ilikaribishwa pia na mashirika ya Kipalestina, ambayo yanaona kuwa ni matunda ya uthabiti wao, kana kwamba Palestina imekombolewa na na umbile la Kiyahudi kung'olewa!

Soma zaidi...

Umbile la Kiyahudi ndilo Tatizo Kubwa zaidi katika Nchi za Kiislamu Na Waungaji Mkono wake ndio Tatizo Kubwa Zaidi Duniani Ewe Trump!

Vyombo vya habari viliripoti taarifa ya Rais wa Marekani Donald Trump kuhusu Gaza, ambapo alisema, “Gaza ni tatizo kubwa kwa Israel na Mashariki ya Kati.” Hatujamsikia hata mmoja wa watawala wajinga wasio na maana (ruwaibidha) katika nchi za Kiislamu akimjibu, akimwambia kwamba umbile nyakuzi la Kiyahudi ndilo tatizo kubwa katika nchi za Kiislamu, na kwamba nyinyi ndio mnaliruzuku zana za kijeshi na msaada wa kisiasa na kiuchumi. Nyinyi ndio tatizo kubwa katika ulimwengu wote. Mfumo wenu wa kibepari ndiyo sababu ya masaibu ya dunia, na nyinyi ndio sababu ya kugawanyika kwa nchi za Kiislamu katika dola dhaifu na maumbo hafifi tiifu kwenu.

Soma zaidi...

Enyi Waislamu: Je, bado mna matumaini kwa Watawala wenu Ruwaibidha?!

Umbile la Kiyahudi bado linatekeleza uhalifu wake dhidi ya watu wa Gaza, hivyo makumi ya mashahidi huongezeka kutokana nao kila siku. Pia bado linapiga mzingiro wake juu ya Gaza, hivyo watu wake wanakufa kwa njaa, kwa kuwa hawana chakula, vinywaji, dawa, au makao, licha ya jitihada fulani za kupeleka misaada kwao kwa uoga! Lakini mamia ya maelfu hawapati tonge ambalo kwalo wanaweza kuzuia njaa zao au kunyamazisha njaa ya watoto wao, kwa hiyo wamekuwa wanakufa kwa njaa mbele yao na mbele ya macho ya ulimwengu wote bila msaidizi au mwenye kuwanusuru.

Soma zaidi...

Enyi Waislamu: Yaelekezeni macho yenu kwenye makasri ya watawala wenu, sio Ikulu ya White House!

Macho ya Waislamu kwa jumla, na waandishi wa habari, wachambuzi, waangalizi, na wale wanaohusika hasa, yanaelekea Ikulu ya White House, na kwenye matokeo ya mikutano ya Rais wa Marekani Donald Trump na Waziri Mkuu wa umbile la Kiyahudi, Benjamin Netanyahu. Je, Trump atamshinikiza Netanyahu kukubali kwa upole kusitisha vita vyake dhidi ya Gaza?

Soma zaidi...

Trump na Netanyahu Wanajigamba na Kujisifu Huku Watawala Wetu Wakikaa Kimya Mithili ya Wafu Makaburini Mwao!

Vita kati ya Iran na umbile la Kiyahudi vimemalizika, na jinai za Mayahudi mjini Gaza hazikukoma wakati wa vita hivyo, wala hadi wakati huu. Marekani ilifanya ujanja wa kiusanii, ikidai kuwa imeangamiza uwezo wa nyuklia wa Iran. Hatua hii imekuja baada ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran kukutana na wale wanaojiita mawaziri wa Troika wa Ulaya, ambao walikuwa sehemu ya mazungumzo ya nyuklia ya Iran kabla ya Marekani kujitoa katika mazungumzo hayo wakati wa muhula wa kwanza wa Trump. Iran pia ilifanya mbwembwe za kiusanii kwa kurusha makombora kadhaa katika Kambi ya Kimarekani ya Al Udeid nchini Qatar, baada ya kuifahamisha Marekani kuhusu hilo, kama Trump mwenyewe alivyosema.

Soma zaidi...

Serikali ya Hindutva ya India Inaendelea Kutumia Shirika la Kitaifa la Uchunguzi kwa Kazi yake Chafu

Mnamo tarehe 14 Juni 2025, Shirika  la Kitaifa la Uchunguzi (NIA) lilifanya uvamizi ulioratibiwa katika maeneo matatu huko Bhopal, Madhya Pradesh, na miwili huko Jhalawar, Rajasthan, kuhusiana na kesi ya Hizb ut Tahrir (HuT). Operesheni hiyo ililenga kukusanya ushahidi zaidi dhidi ya HuT. NIA ilidai kuwa uvamizi huu ulisababisha kukamatwa kwa "vifaa vya kidijitali na nyenzo za hatia" (vitabu na vifaa vya kuandikia tunavyodhania). Kabla ya uvamizi huu, Jharkhand (jimbo) ATS ilikuwa imewaweka kizuizini watu wawili kuhusiana na kesi ya Hizb ut Tahrir. Serikali ya India ilipiga marufuku kinyume cha sheria Hizb ut Tahrir mnamo tarehe 10 Oktoba 2024, ikitaja juhudi zake za kusimamisha "Khilafah" ya kimataifa kupitia ugaidi na itikadi kali.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu