Wanachama wa Hizb ut Tahrir huko Abbasiya Watangaza: Tibueni Mpango wa Amerika wa Kutenganisha Darfur
- Imepeperushwa katika Al-Rayah
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Kama sehemu ya kampeni iliyoandaliwa na Hizb ut Tahrir/Wilayah Sudan kutibua mpango wa kuichana Sudan kwa kutenganisha eneo la Darfur, na kwa kuzingatia kwamba umoja wa Ummah ni suala nyeti, ambalo ni lazima hatua za uhai au kifo zichukuliwe, Mashababu (wanachama) wa Hizb ut Tahrir walifanya mkutano mnamo Ijumaa, 6 Rabi’ al-Awwal 1447 H, sawia 29 Agosti 2025 M, baada ya swala ya Ijumaa, katika Msikiti wa Sheikh Yahya wa Kuhifadhi Qur'an. Walitoa wito wa dhati kwa Waislamu wa makundi yote, wakiwemo wanasiasa, wanahabari, maulamaa, maafisa na wanajeshi, na wengineo, wakiwataka watimize wajibu wao wa Shariah wa kuzuia kujitenga kwa Darfur.