Wahanga wa Vita Wanaoteseka Zaidi ni Watoto wa Gaza wenye Ulemavu
- Imepeperushwa katika Kitengo cha Wanawake Afisi Kuu ya Habari
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Vita vya maafa dhidi ya Gaza, vilivyoanza mnamo Oktoba 7, 2023, vimeathiri kila nyanja ya maisha huko: watu, miti, mawe, na rasilimali, hasa wanawake na watoto. Vifo na uharibifu vimeenea kila mahali. Kulingana na Wizara ya Afya mjini Gaza, vimesababisha vifo vya zaidi ya watu 63,000, kujeruhiwa kwa wengine 160,000, na mamia ya maelfu ya watu kuyahama makaazi yao, huku kukiwa na janga kubwa la kibinadamu linalojumuisha uhaba wa chakula, dawa, na maji safi ya kunywa.